Thursday, May 14, 2015

SERIKALI : MADEREVA ENDELEENI NA UTARATIBU WA ZAMANI KUHUISHA LESENI ZENU.

Share it Please
Serekali imesema hakutakuwa na mafunzo ya udereva kwa madereva wa mabasi na malori wala madereva kutakiwa kwenda kusoma kozi fupi ili kuhuisha leseni zao kama ilivyotangaza hapo mwanzo na kusababisha mgomo wa madereva. Kauli hiyo imetangazwa jana na kamanda wa kikosi cha polisi wa barabrani bw Mohammed Mpinga alipokuwa akitangaza uamuzi huo wa serikali.

mwenyekiti wa madereva clemence masanja akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa kutangaza uamuzi huo mapema jana.

Alisema kuwa madereva wenye madaraja E,C1,C2 na C3 ambao walitakiwa kupitia kozi fupi ya udereva kila baada ya miaka 3 kulingana na kanuni zilizopitishwa mwaka 2014 na mamlaka ya usafirishaji majini na nchi kavu (SUMATRA),mamlaka ya mapato tanzania (TRA), chama cha wamiliki wa mabasi (TABOA), Chuo cha usafirishaji (NIT), chama cha wamiliki wa magari ya mizigo (TATOA),vyama vya madereva na ofisi ya mwanasheria mkuu wa serikali.
Kamanda mpinga alitoa wito kwa madereva kuwa wavumilivu na matatizo yao wakati kamati ya kudumu ya kutatua matatizo katika sekta ya usafirishaji ikiendelea kuyataftia ufumbuzi wa kudumu.
kamanda wa polisi kikosi cha uasalama barabarani mohammed mpinga akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa habari (hawapo pichani)

No comments:

Post a Comment

Followers

Follow The Author