Tuesday, May 26, 2015

ANCELOTTI NJE REAL MADRID.

Share it Please


Baada ya kuitumikia kablu hiyo kwa misimu miwili mfululizo,hatimaye klabu ya real madrid kupitia kwa rais wake florentino perez jana imesitisha kibarua cha kocha wake.
Kocha huyo raia wa Italia, aliiongoza Madrid kutwaa taji la kombe la Hispania kabla ya kuibebesha miamba hiyo taji la kumi la klabu bingwa barani Ulaya. 
Pamoja na mafanikio hayo aliyoyapata msimu uliopita, mwaka huu haukuwa mzuri kwa vijana hao wa Benabeu baada ya kuambulia patupu kwa kukosa hata kombe moja japokuwa kikosi cha timu hiyo kinatajwa kuwa cha gharama ya juu. Hasira za viongozi wa klabu hiyo ziliongezeka baada ya kutupwa nje na Juventus katika hatua ya nusu fainali ya klabu bingwa Ulaya huku wapinzani wao wakubwa Barcelona ikinyakuwa taji la ligi kuu na kutinga fainali ya klabu bingwa na kombe la Hispania. 
Rais wa Madrid Florentino Perez amewaambia waandishi wa habari kuwa haikuwa rahis kumtema kocha huyo na kuongeza kuwa kocha mpya atateuliwa wiki ijayo. Makocha jurgen kloop na Raphael Benitez wanapewa nafasi kubwa ya kunyakua kiti hicho.

No comments:

Post a Comment

Followers

Follow The Author