Tuesday, May 26, 2015

SAFARI YA MATUMAINI KUANZIA ARUSHA JUMAMOSI HII TAR 30/05/2015

Share it Please
Jumamosi hii ya tarehe 30/05/2015, Waziri mkuu wa zamani na mbunge wa Monduli Mh Edward Lowassa atazungumza na watanzania kwenye viwanja vya Sheikh Amri Abeid Arusha kuanzia saa nane mchana. Hii ni katika kuelekea KUANZA kwa ile anayooita "safari ya matumaini"  ambapo anatarajiwa kutangaza rasmi nia yake ya kugombea nafasi ya uraisi wa jamhuri ya muungano wa Tanzania kupitia chama cha mapinduzi (CCM).
Mh Lowassa aliyasema hayo juzi kwenye kikao chake na wahariri wa vyombo vya habari kilichofanyika nyumbani kwake Dodoma ambapo aliongelea mambo mbali mbali ikiwemo afya yake,sakata la richmond, utajiri wake na pia hali ya kisiasa nchi Tanzania kwa sasa. Katika kikao hicho mh Lowassa alitoa ufafanuzi wa mambo hayo ikiwemo kukaa kwake kimya kwa takribani miaka 7 kwenye nyanja ya siasa na kuahidi kutangaza rasmi azma yake ya kugombea nafasi hiyo nyeti na kubwa kwa taifa siku ya jumamosi ya tarehe 30/05/2015 katika viwanja vya Sheikh Amri abeid Arusha.

No comments:

Post a Comment

Followers

Follow The Author