
muonekano wa uwanja wa Sheikh Amri Abeid baada ya maandalizi.
Jiji la Arusha na viunga vyake limeendelea kupokea na kufurika wageni mbali mbali kutoka sehemu tofauti Tanzania wanaotarajiwa kuhudhuria kwenye mkutano mkubwa ambapo aliyekuwa waziri mkuu wa jamhuri ya muungano wa Tanzania na mbunge wa Monduli kwa tiketi ya chama cha mapinduzi mh Edward Ngoyai Lowassa anatarajiwa kutangaza rasmi nia yake ya kugombea nafasi ya uraisi kwa tiketi ya CCM kweye uchaguzi mkuu utkaofanyika mapema oktoba 25 mwaka huu.
Baadhi ya wadau wa team lowassa wakiwa ndani ya uwanja wa Sheikh Amri Abeid kukamilisha maandalizi ya mkutano huo.

gari ikipita mtaani kutangaza mkutano huo.

moja ya majukwaa yatakayotumika.

team Lowassa ndani ya t shirts.
Mapema siku chache zilizopita,kwenye kikao chake na wahariri wa vyombo vya habari kilichofanyika nyumbani kwake mjini Dodoma, mh Lowassa aliahidi kutangaza nia yake ya kugombea nafasi hiyo jumamosi hii katika viwanja hivyo vya sheikh amri abeid.
No comments:
Post a Comment