Wednesday, May 27, 2015

CHAMA CHA WALIMU TANZANIA (CWT) KUFANYA UCHAGUZI WAKE KITAIFA KESHO MJINI ARUSHA.

Share it Please
Chama cha walimu nchini tanzania (CWT) kinatarajia kufanya uchaguzi wake kesho mjini arusha ili kupata viongozi wa kitaifa wa chama hicho watakaoongoza chama hicho kwa kipindi cha miaka  mitano.
Tayari mkutano mkuu wa chama hicho umefunguliwa leo jijini arusha katika hoteli ya Ngurdoto kwa hotuba ya rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Dk, Jakaya M. Kikwete ambapo ameahidi kutatua changamoto zinazowakumba walimu kabla ya kuondoka madarakani oktoba mwaka huu.

Raisi kikwete akiwasili ukumbini kufungua mkutano huo.
kjj1
raisi kikwete akihutubia walimu wakati wa  ufunguzi wa mkutano huo.

Jumla ya walimu zaidi ya 1000 kutoka sehemeu mbalimbali Tanzania wametarajiwa kuhudhuria mkutano huo ambapo katika uchaguzi huo walimu wanatarajia kuchagua viongozi katika ngazi za Mwenyekiti, katibu naibu katibu na mhazini.
mr2
Rais kikwete akiteta jambo na mmoja wa waasisi wa chama cha walimu tanzania (CWT) ndugu Thom abieko

No comments:

Post a Comment

Followers

Follow The Author