Mkusanyiko mkubwa wa wafanyabaishara hao ulionekana maeneo ya ilala kwenye makutano ya barabara ya kawawa na uhuru jirani na zilipo ofisi za mkuu wa mkoa wa dar es salaam ambapo ndipo hasa walitaka uongozi wa mkoa na wilaya ya ilala watoe maelezo juu ya kuvunjwa kwa mabanda yao ya biashara.
baadhi ya walemavu waliokuwa sehemu ya mgomo huo
foleni ya magari iliyosababishwa na mgomo huo.

baadhi ya walemavu wakiwa wamefunga makutano ya barabara ya uhuru na kawawa mapema leo.
Mgomo huo wa walemavu uliodumu kwa masaa matatu ulihitimishwa baada ya mkuu wa wilaya ya ilala mh Raymond Mushi kuahidi kuwa manispaa ya ilala itafanya uchunguzi ili kubaini kama kuna uharibifu uliotokea na kulipa fidia kwa wahanga.
No comments:
Post a Comment