Thursday, May 21, 2015

NEWS! WALEMAVU WAANDAMANA NA KUFUNGA BARABARA DAR!

Share it Please
Kundi la walemavu wajasiriamali kutoka umoja wa wafanya biashara wenye ulemavu dar  (uwawada) leo wamefanya maandamano yaliyopelekea kufunga barabara kadhaa katika mkoaa wa dar wakishinikiza serikali kutoa maelezo juu ya uvunjaji wa meza za biashara katika soko la machinga complex la ilala dar es salaam unaodaiwa kufanywa na askari wa jiji usiku wa kuamkia jana.

Mkusanyiko mkubwa wa wafanyabaishara hao ulionekana maeneo ya ilala kwenye makutano ya barabara ya kawawa na uhuru jirani na zilipo ofisi za mkuu wa mkoa wa dar es salaam ambapo ndipo hasa walitaka uongozi wa mkoa na wilaya ya ilala watoe maelezo juu ya kuvunjwa kwa mabanda yao ya biashara.
baadhi ya walemavu waliokuwa sehemu ya mgomo huo


foleni ya magari iliyosababishwa na mgomo huo.

Baadhi ya walemavu hao wakionekana kufunga pande mbili za makutano ya barabara hizo za Kawawa na Uhuru jijini  Dar Es Salaam. Picha na MichuziBlog.
baadhi ya walemavu wakiwa wamefunga makutano ya barabara ya uhuru na kawawa mapema leo.

Mgomo huo wa walemavu uliodumu kwa masaa matatu ulihitimishwa baada ya mkuu wa wilaya ya ilala mh Raymond Mushi kuahidi kuwa manispaa ya ilala itafanya uchunguzi ili kubaini kama kuna uharibifu uliotokea na kulipa fidia kwa wahanga.

No comments:

Post a Comment

Followers

Follow The Author