Monday, May 25, 2015

DROGBA AAGA RASMI CHELSEA.

Share it Please



Ikiwa Ligi kuu ya Uingereza imekwisha huku timu ya Chelsea wakiwa mabingwa wa msimu huu, mshambuliaji wa klabu hio Didier Drogba amefanya maamuzi magumu juu ya maisha yake ya soka na klabu hio.
Drogba atawaacha Mashabiki wa Chelsea watakuwa na furaha baada ya kuwa mabingwa lakini wakati huo huo watakuwa na huzuni ya kumpoteza mshambuliaji wao kipenzi Didier Drogba ambaye ametangaza kuiacha klabu hio na kwamba hii ndio mechi yake ya mwisho.
Drogba aliandika ujumbe kupitia account yake ya Instagram kuwa ” Nimezungumza na kocha wangu Jose Mourinho kuhusu hatma yangu kuwa nataka kuendelea kucheza soka hata msimu moja na ili nicheze zaidi soka lazima niende timu nyingine” aliongeza "mashabiki wa klabu hii wanafahamu mapenzi niliyonayo juu ya klabu na natamani kurudi tena hapa siku moja lakini kwa nafasi nyengine".
Drogba anamiaka 37 alijiunga kwa mara ya kwanza na Chelsea mwaka 2004 na kuwepo kwenye klabu hiyo kwa takribani misimu minane yenye mafanikio ambapo ameifungia klabu ya chelsea jumla ya magoli 104  kwenye mechi 253 za ligi. Kwa msimu huu drogba ameifungia klabu hiyo magoli saba (7) tangu kujiunga kwake kwa mkataba mfupi wa mwaka mmoja.
Screenshot_2015-05-24-15-24-10

No comments:

Post a Comment

Followers

Follow The Author