Wednesday, May 27, 2015

RAIS OBAMA KUPATA MKWE KENYA ?.... WAKILI KUTOKA KENYA ATANGAZA NIA KUMCHUMBIA MTOTO WAKE.

Share it Please
obama akiwa na mtoto wake wa kike, malia obama
Habari kubwa iliyotawala tasnia ya habari duniani leo ni kuhusu Wakili kutoka nchini kenya Felix kiprono amabye ameushangaza umma baada ya kutangaza nia yake ya kutoa posa ili kumuoa mtoto wa raisi wa marekani,malia Obama mwenye umri wa miaka 16.
Taarifa zinasema kuwa wakili huyo wa kenya amesema yuko tayari kutoa mahari kwa mtoto wa raisi wa Marekani na atatoa ng'ombe 50,kondoo 70 na mbuzi 30 kwa ajili ya mahari ya mtoto wa Obama,Malia Obama.
felix kiprono,wakili aliyetangaza nia kumuoa mtoto wa obama, Malia obama.

Felix amesema anajiandaa kuzungumzia swala hilo na baba wa mtoto huyo atakapo tembelea Kenya ,mwezi Julai. Rais Obama atakuwa na ziara ya kikazi nchini kenya ambapo atatua nchini humo tar 25 ya mwezi wa saba(july) na kuhutubia kwenye mkutano wa dunia kuhusu ujasiriamali, mkutano unaotarajiwa kuwakutanisha wafanyabiashara na wamiliki wa viwanda kutoka duniani kote,

No comments:

Post a Comment

Followers

Follow The Author