Friday, June 12, 2015

SAFARI YA MATUMAINI YAENDELEA TENA SHINYANGA. AVUNJA REKODI YA KUPATA WADHAMINI WENGI.

Share it Please
Waziri Mkuu wa zamani na Mbunge wa Monduli, Mh. Edward Lowassa, akisalimiana na mtoto mwenye ualbino, Kabula Zacharia, anayetunzwa kwenye kituo cha kulea watu wenye mahitaji maalum cha Buhangija mkoani Shinyanga, mara baada ya kupata wana CCM wa kumdhamini kufuatia kuchukua fomu za kuomba chama kimteue kuwania urais wa Tanzania kwenye uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 25, 2015. Mh. Lowassa ambaye yuko kanda ya ziwa kutafuta wadhamini, alivunja rekodi ya kupata wadhamini 7,114, idadi kubwa hadi sasa. (Picha na K-VIS MEDIA)
Mh. Lowassa, akipokea fomu zilizojazwa na wana CCM waliomdhamini mkoani Shinyanga, kutoka kwa katibu wa CCM wilaya ya Shin yanga mjini Charles Sangula, Juni 11, 2015.
Waziri Mkuu wa zamani na Mbunge wa Monduli, Mh. Edward Lowassa, akipungia mkono wana CCM na wananchi wa Mkoa wa Shinyanga, alipokuwa akiondoka ofisi za chama hicho wilaya ya Shinyanga mjini mara baada ya kupata wana CCM wa kumdhamini baada ya kuchukua fomu kuomba CCM imteue kugombea urais kwenye uchaguzi mkuu wa Tanzania unaotarajiwa kufanyika Oktoba 25, 2015. Mh. Lowassa amabaye yuko kanda ya ziwa kutafuta wadhamini, alivunja rekodi ya kupatya wadhamini 7,114, idadi kubwa hadi sasa

No comments:

Post a Comment

Followers

Follow The Author