Mshindi wa Shindano la Bongo Star Search 2015 (BSS), Kayumba Juma (katika), akiwa ameshikilia fedha zake muda mfupi baada ya kuibuka kidedea kwenye fainali hizo zilizokuwa zikifanyika usiku wa kuamkia leo katika Ukumbi wa King Solomoni uliopo Namanga jijini Dar es Salaa.
Jaji Mkuu wa mashindano hayo, Madam Rita (wa pili kutoka kushoto), akimtangaza mshindi huyo.
Washiriki waliongia kwenye 6 bora ya mashindano hayo wakiwa jukwaani kabla ya mchujo huo kuanz
Mmoja wa Majaji wa shindano hilo (kulia), Master Jay akiingia ukumbini hapo huku akiwa ameongozana na mpenzi wake ambaye ni msanii wa Bongo fleva Shaa.
Majaji wakiwa kwenye meza yao ya kuratibia mashindano hayo.
Peter Msechu akiwa katika pozi kwenye Red Carpet.
Wasnii wanaounga kundi la Navy Kenzo wakipagawisha jukwaani hapo.
Msanii Kayumba Juma, usiku wa kuamkia jana aliibuka mshindi katika kinyang'anyiro cha kumsaka msanii mwenye kipaji cha kuimba kinachojulikana kama Bongo Star Search baada ya kuwabwaga wenzake watano waliofanikiwa kuingia katika sita bora ya kinyang'anyiro hicho na hivyo kufanikiwa kujinyakulia zawadi ya shilingi millioni 50 kutoka kwa waandaaji wa shindano hilo.
Kayumba aliwabwaga chipukizi wengienwatano ambao ni Frida Amani, Nassibu Fonabo, Jcqueline kayengi, Angel Marry Kato na Kelvin Gerson.
Mashindano hayo yanaandaliwa na kampuni ya Benchmark Production chini ya ukurugenzi wa Ritha Poulsen "Madam Ritha" amabaye ni chief judge wa mashindano hayo yanafanyika kwa mara ya 8 yakianzia mwaka 2006 ambapo jumanne Idd alifanikiwa kunyakua ubingwa kwa mara ya kwanza.
Mbali na kitita hicho cha million 50, Kayumba pia amefanikiwa kupata bure bima ya afya kwa mwaka mmoja chini ya Jubilee Insurance.
No comments:
Post a Comment