Jurgen kloop akiwa ameshikilia skafu ya Liverpool Mara baada ya kutambulishwa kwa waandishi wa habari.
Klabu ya soka ya Liverpool imemteua Jurgen Klopp kuwa kocha wake mpya kwa mkataba wa miaka mitatu.
Klopp, raia wa Ujerumani mwenye miaka 48 anachukua nafasi ya Brendan Rodgers aliyetimuliwa hivi karibuni baada ya kuhudumu katika klabu hiyo kwa miaka mitatu na nusu.
Klopp amekuwa nje ya dimba tokea mwezi Mei mwaka huu baada ya kudumu na klabu ya Borussia Dortmund kwa misimu saba.
Anatarajiwa kuanza kazi kwenye klabu hiyo ya Liverpool na wasaidizi wake Zeljko Buvac na Peter Krawietz aliofanya nao kazi akiwa kwenye Ligi ya Bundesliga.
.Kloop Alijiunga Dortmund mwaka 2008 na kuiongoza kushinda vikombe viwili vya ligi kuu ya Ujerumani (Bundesliga).
Klopp, raia wa Ujerumani mwenye miaka 48 anachukua nafasi ya Brendan Rodgers aliyetimuliwa hivi karibuni baada ya kuhudumu katika klabu hiyo kwa miaka mitatu na nusu.
Klopp amekuwa nje ya dimba tokea mwezi Mei mwaka huu baada ya kudumu na klabu ya Borussia Dortmund kwa misimu saba.
Anatarajiwa kuanza kazi kwenye klabu hiyo ya Liverpool na wasaidizi wake Zeljko Buvac na Peter Krawietz aliofanya nao kazi akiwa kwenye Ligi ya Bundesliga.
.Kloop Alijiunga Dortmund mwaka 2008 na kuiongoza kushinda vikombe viwili vya ligi kuu ya Ujerumani (Bundesliga).
Wakati Kloop akisaini kuifundisha klabu hiyo, aliyekuwa kocha wa zamani wa manchester united Sir Alex Ferguson amezungumzia uteuzi huo.
Sir Ferguson alisema “Ni uteuzi mzuri, namjua vizuri kupitia kwenye mikutano yetu ya darasa la ukocha tukiwa Geneva. Klopp ni mtu makini na pia anapenda kujua kila kitu na kujaribu kukitumia kwenye kazi. Pia anajua nini anakitaka akiwa na mipango yake kama tulivyoona alivyofanya vizuri na Dortmund. Nadhani atafanya vizuri, sitaki kusema hivyo kwasababu ni Liverpool lakini bila shaka lazima atafanya vizuri”
Fergie aliongeza kusema kwamba ni vizuri kama Klopp akifanya kazi mwenyewe bila kuingiliwa na wamiliki, “Kama haumuamini manager wako sasa utamuamini nani? Huyu ndio mtu pekee anatakiwa kusema mchezaji anamtaka na akacheze wapi. Kuna haya mambo ya kibiashara sana kwenye soka, nadhani kuna wakati yanakosewa. Kama haumuamini kocha kwanini umempa kazi. Sidhani kama Klopp atalikubali hili swala”
No comments:
Post a Comment