Wednesday, August 31, 2016

SIRI UNAYOTAKIWA KUIJUA WEWE MKE AU MUME, by Dr Chris Mauki (phd in psychology)

msaidie
(Mentor wangu Myles Munroe RIP alinisaidia kitu, nadhani nikiweka mkazo kitakusaidia na wewe)
Yako mambo ambayo ni muhimu kukumbuka katika suala zima la kutoa na kupokea baina ya mume na mke katika ndoa. Mwanaume anapoonyesha kutaka au kuhitaji kitu kutoka kwa mwanamke, mwanamke huhamaki, wakati mwanaume akitoa kitu kumpa mwanamke, mwanamke huitika kwa hujisogeza karibu na mwanaume (hapa namaanisha kuwa mwanamke anapopokea kitu kutoka kwa mwanaume yeye hujikuta anaongeza kuwa karibu zaidi na mwanaume huyu kuliko wakati ambao mwanamke ndiye anayempa kitu mwanaume). Katika asili hii utaona uhalisi wa mwanaume kumtimizia mahitaji mwanamke na sio mwanamke kumtimizia au kumtunza mwanaume (ni jambo la asili mwanaume kumpa mahitaji mwanamke na sio mwanamke kumpa mahitaji mwanaume). Mwanaume anapojitoa kwa moyo kwa ajili ya mwanamke, mwanamke kunyenyekea bila shuruti. Hakuna kilicho cha thamani sana kwa mwanamke zaidi ya mwanaume mwenye uwezo wa kujitoa kwa moyo wa dhati kwa ajili ya mke wake. Hakuna kinacho muumiza na kumkatisha tamaa mwanamke kama kuwa na mwanaume asiyeweza kujitoa kwa moyo wa dhati kwa ajili ya mke wake. Ngoja nikushirikishe siri iliyopo hapa; Kama unatamani kuwa na mwanamke mnyenyekevu basi jifunze kujitoa kwa moyo wa dhati kwake, unapoonyesha kutaka kumuumiza mkeo, mkeo naye kuonyesha kujihami au kukukwepa. Pale mwanaume anapomshirikisha mwanamke na mwanamke naye huongeza kumjali mwanaume. Mwanaume anapoonyesha kuongoza, kwa uongozi wenye uwajibikaji, basi na mwanamke naye huonyesha kufuata uongozi ule. Uongozi hapa simaanishi kuwa bosi wa mkeo, kila siku unatoa amri za nini unataka kifanywe na kifanywe vipi, la hasha, kwa kuwa kiongozi hapa namaanisha kutangulia mbele na kuwaonyesha wengine njia, sio wewe kuwaweka wengine mbele wakati wewe unakwepa au unahofia hatari. Kuongoza hapa namaanisha kumwonyesha mwenza wako namna bora ya kufanya au namna bora ya kuenenda. Ukisema hutaki kitu fulani basi unaonyesha kwa vitendo nini unachokitaka na kwanamna gani unakitaka kiwe au kifanywe. Hapa namaanisha kuongoza kwa mifano (leading by examples). Ukiwachunguza viongozi wote wa kwenye vitabu vitakatifu, iwe Biblia au hata Quran, utagundua kwamba wote waliongoza kwa mifano. Fahamu hili na ulizingatie litakusaidia sana.
Continue Reading...

MASAUNI AZINDUA PROGRAMU YA “TUNZA AMANI IKUTUNZE” JIJINI DAR ES SALAAM

Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akionyesha Kitabu, DVD na CD zenye ujumbe wa “TUNZA AMANI IKUTUNZE”, wakati wa uzinduzi wa mkakati huo wenye lengo la kudumisha amani ulioratibiwa na Shirika la Kukuza Amani na Uchumi Tanzania(PSEDO) , Kulia ni Mkurugenzi wa shirika hilo, Askofu Nason Ngoy Ngoy. Hafla hiyo imefanyika   leo katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Mwalimu Julius Nyerere, jijini Dar es salaam.


 Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni akizungumza mara baada ya uzinduzi wa  Kitabu, DVD na CD zenye ujumbe wa “TUNZA AMANI IKUTUNZE”, wakati wa uzinduzi wa mkakati huo wenye lengo la kudumisha amani ulioratibiwa na Shirika la Kukuza Amani na Uchumi Tanzania(PSEDO). Hafla hiyo imefanyika  leo katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Mwalimu Julius Nyerere, jijini Dar es salaam

             Mkurugenzi wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu(LHRC), Dk. Hellen Kijo Bisimba akizungumza mara baada ya uzinduzi wa  Kitabu, DVD na CD zenye ujumbe wa “TUNZA AMANI IKUTUNZE”, wakati wa uzinduzi wa mkakati huo wenye lengo la kudumisha amani ulioratibiwa na Shirika la Kukuza Amani na Uchumi Tanzania (PSEDO). Hafla hiyo imefanyika  leo katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Mwalimu Julius Nyerere, jijini Dar es salaam.

                 Mkurugenzi wa Shirika la Kukuza Amani na Uchumi Tanzania (PSEDO).  Askofu Nason Ngoy Ngoy, akizungumza wakati wa  uzinduzi wa Kitabu, DVD na CD zenye ujumbe wa “TUNZA AMANI IKUTUNZE. Hafla hiyo imefanyika  leo katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Mwalimu Julius Nyerere, jijini Dar es salaam.

               Washiriki wa uzinduzi wa Kitabu, DVD na CD zenye ujumbe wa “TUNZA AMANI IKUTUNZE”, ulioratibiwa na Shirika la Kukuza Amani na Uchumi Tanzania(PSEDO), wakimsikiliza Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni(hayupo pichani) wakati wa hafla hiyo iliyofanyika leo katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Mwalimu Julius Nyerere, jijini Dar es salaam

Continue Reading...

Followers

Follow The Author